1. Onjeni mwone kwamba Bwana yu mwema, na heri yule mtu anayemtumaini Yesu Kristu.
Pokea moyo wangu, ee Mungu wangu, niweze kukupenda kwa pendo lako, (unipe moyo wako, ewe Yesu Mkombozi wangu, shinda kwangu nami daima kwako) x 2.
2. Katika nguvu za giza katutoa na kutukaribisha katika ufalme wa pendo lake.
3. Habari njema alituhubiria na kutufungulia, akatangaza mwaka wa neema.
4. Mchungaji wangu mkuu ndiye Bwana Yesu, sikosi kitu kamwe, huniongoza kwenye njia nyofu.
5. Baraka na heshima na utukufu na uwezo kwa yeye Mwana Kondoo wa Mungu milele.
댓글