Pasipo makosa Mkombozi wetu, Katika baraza la wakosefu Na wote walia asulibiwe, Aachwe Baraba na Yesu afe Aachwe Baraba na Yesu afe
Ee Yesu washika msalaba wako, Na unakubali kufa juu yake Ee Yesu useme sababu gani, Ya nini mateso makali hayo? Ya nini mateso makali hayo?
"Ni pendo kwa Baba wa uwinguni, Ni huruma yangu kwa wakosefu. Ewe mkristu kumbuka mateso yangu, Uache makosa, uache dhambi Uache makosa, uache dhambi"
top of page
bottom of page
コメント