Pana mahali pazuri mno, Twapaona kwa mbali sasa;
Baba yetu angoja pale, Amepanga makao yetu.
Kitambo tu bado, Tutakutana ng`ambo pale.
Kitambo tu bado, Tutakutana ng`ambo pale.
Tutaimba pale kwa moyo Nyimbo tamu za wenye heri.
Na rohoni hatutaona Tena haja ya kupumzika.
Kwa baba yetu mkarimu Tutatoa shukrani sana.
Kwa kipaji cha pendo lake Na baraka anazotupa.
Comments