Palikuwa na kijana mmoja jina lake Samweli, Alikuwa akimcha Mungu tangu utoto wake Alisikia sauti Ikimwita, Samweli, Samweli x2
Alikuwa 'kiitwa na Mungu, lakini hakujua, alikimbilia kwake Eli, Eli hakuelewa
Aliitwa naye Mungu tena, wala hakufahamu, Eli 'kashangaa akasema: Mimi sikukuita
Alipoitwa mara ya tatu, Samweli akajibu: Nena, Bwana, mtumishi wako anatega sikio.
Mungu akawa pamoja naye, na Israeli nzima ikafahamu kuwa Samweli ndiye nabii wake
Comments