Mungu wangu nikujue mimi, Mungu wangu nikupende Mungu nikutumikie, kisha niurithi ufalme Mbinguni x2 (wewe) roho umenipa ee, (kisha) ukaihifadhi vizuri (yaani) ndani ya mwili ee (kwani) mwili ni nyumba ya roho
Ndiwe mungu peke yako, wa kuabudiwa ni wewe nishike kitakatifu siku hiyo siku yako nisilitaje kabisa bure jina lako Mwenyezi Ulimi wa mwili wangu usiiponze roho yangu
Niwaheshimu wazazi, ili nisiwasononeshe uhai wa binadamu niuthamini yani nisiuue kuiba nijiepushe, kusema uwongo niache Mwili wangu usizini ndipo roho yangu itapona
Niepuke kutamani yote yasiyo mali yangu naye mwanamke asiye mke wangu yani sio wangu Hapo ndipo nitakuwa nimeutumia vizuri mwili ulioiumbia roho ifike Mbinguni juu
Comments