Kakukirimia, uwe ulivyo, Atakutumia impendezavyo Akikuinua, inuka, hivyo, Ninakuombea heri vilivyo; Hakunipa hayo, nikuhitaji, Kwa niliyo nayo, upate maji, Na mwisho wa hayo, tuvikwe taji, Tuingie nayo, wa mbingu mji.
Sirudi kwa njia, yake herode, Anakuvizia, kila upande, Wivu unamjia, kakunja, konde, la kukuzuia juu usipande; Ni kama Kaini, mwua Abeli, au Raubeni, wa Israeli, Waliotamani, kuzika, hali, Ya wadogo duni, wake Jalali!
Ninakuombea, usife moyo, Maana dunia, si rafikiyo, Wewe fuatia, za Kristu, nyayo, Aliyekufia, kwa mizigoyo; Wa ulimwenguni, watakufumba,Wazuri machoni, moyo mwembamba, Hawatatamani, uitwe, mwamba,Ni wivu moyoni, unawasomba!
top of page
bottom of page
Comments