Tutamsifu Mungu, tutamwimbia Watunzi tutampangia nota mpaka mbinguni
Usiku na mchana, jioni na asubuhi Kiangazi masika mpaka Mbinguni
Tumetafiti tukauliza, maandiko tukafunua Kutambua watakatifu, wanafanya kazi gani Mbinguni
Enyi wasomi tuambieni, wanasayansi tujibuni Katika mambo ya mbinguni, nini kinafanyika duniani
Tumetambua kule mbinguni, hakuna kwenda ofisini Wala kumbi za burudani, hata kilimo hakuna lakini
Kumbe furaha za dunia hii, ni upumbafu ni wazimu Na anasa za maadili, sisi waimbaji tumeamua
Waamini wote furahini, makasisi shangilieni Nanyi watawa jiungeni, kwa waimbaji hakuna matata
Upendo wake ni wa ajabu, fadhili zake za milele Huruma yake ni amini, msamaha wake unashangaza
留言