Nitatoa nini mimi Ewe Mungu wangu Kitakacho kuwa sawa na fadhili zako Wewe ni Bwanawa rehema Fadhili zako za milele Nikupe nini nikupe nikushuru Kama ni fedha nazo ni zako Hata mazao -ya shambani Nikupe nini nikupe nikushukuru
Mema mengi umenitendea ee Mungu wangu, hata siwezi kukulipa, mara ngapi nimekukosea ee Mungu wangu, na wewe ukanisamehe.
Usiku hata mchana wewe umenilinda, hata hivyo sikushukuru, umenilisha chakula ili nipate nguvu, hata hivyo sikushukuru
Ninajitolea kwako kimwili na kiroho, kazi hata maisha yangu, nitaimba nikisema asante Mungu wangu, siku zote hata milele.
Comments