Nitalisifu Jina lake Mungu kwa wimbo wangu, nami nitamshukuru yeye siku zote, kwa sababu Bwana ananipenda daima, amenipa uzima na amenibariki x2
Watu wote njooni leo Tuimbe kwa shangwe, mbingu na dunia njoni Tuimbe kwa shangwe, njoni mbele zake Bwana Tuimbe kwa shangwe
Tangazeni sifa zake Bwana anatupenda, hubirini pande zote Bwana anatupenda, lisifuni Jina lake Bwana anatupenda
Bwana ametuokoa Ametubariki, ametupa vitu vyote Ametubariki, ametulinda salama Ametubariki
Nguvu enzi na uwezo Ni wake milele, nguvu-u na utawala Ni wake milele, madaraka na ufalme Ni wake milele
Comments