top of page

Nitakuandama Kote

Nitakuandama kote, nitakapoagizwa

Wewe ukiniongoza nami nitaandama.


Nitakuandama kote, naam, ulinifia;

Kwa neema yako Bwana napenda kuandama.


Njia ijapoparuza kwa miiba na fujo,

Ulitangulia mbele nami nitaandama.


Nijapokuta taabu na majaribu kote,

Nakumbuka shida yako, nami nitaandama.


Nijapoona ukiwa na mateso makali,

Wewe uliyatikiza nami nitaandama.


Ijapo wanipeleka vilindini mwa giza,

Wewe uliyetikiza nami nitaandama.

10 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page