Nitaimba na kumtukuza muumba wangu hata nizeeke, nitembee na fimbo, nitembee na fimbo ili nimsifu Bwana Mungu wangu x2
Mama Maria nakubembeleza, Mama Maria unisaidie, uniombee (Mama) kwa Mwanao Yesu, niishi siku nyingi (ili) nimsifu Bwana x2
Nitalitangaza neno la Bwana bila aibu, milele na milele mpaka nitembee na fimbo.
Nitalihubiri neno pande zote ulimwenguni, milele na milele mpaka nitembee na fimbo.
Atukuzwe Baba na Mwana nae Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote na milele.
Comments