Niseme nini ee Bwana, nitamke maneno gani kinywani nikushukuru jinsi gani, nisimulie vipi mimi, mapito niliyopita kuja hapa nikutukuze vipi Mungu Niseme tu, Bwana Mungu wangu, asante nakushukuru narudia, Bwana Mungu wangu, asante nakushukuru
Nakumbuka nilivyojaribu, sikujua kama utajibu nikapapasa mkono kizani, kulipokucha ni tunda mkononi
Katikati ya safari maji yale yakamwagika chini lakini kwa wema wako, umeyazoa yakajaa upya
Nilipigwa mawe nikaaibishwa sana tazama leo umeniona, ukamtukuza mtumishi wako
Comentarios