top of page

Nisamehe Bwana


  1. Nisamehe Bwana mimi mtumishi wako, naja mbele yako naja na sala yangu, ninanyenyekea chini ya miguu yako, unitakase kwa makosa yangu yote

  2. Sistahili mimi kuikaribia meza, wala hata kunena jambo lolote, nimejuta sana naomba huruma yako, unipokee mimi mtumishi wako

  3. Ninapokuomba Bwana unisikilize, mahangaiko ya dunia mengi sana, yamenisonga kushoto hata kulia, mbele mbele na nyuma mimi sioni kitu

  4. Ndugu zangu nao wananichekelea, ninapopambana na hali hali zangu, hivyo tumaini langu naliweka kwako, njoo hima Bwana wangu uniokoe

4 views0 comments

Comentarios

Obtuvo 0 de 5 estrellas.
Aún no hay calificaciones

Agrega una calificación
bottom of page