Nisamehe Bwana mimi mtumishi wako, naja mbele yako naja na sala yangu, ninanyenyekea chini ya miguu yako, unitakase kwa makosa yangu yote
Sistahili mimi kuikaribia meza, wala hata kunena jambo lolote, nimejuta sana naomba huruma yako, unipokee mimi mtumishi wako
Ninapokuomba Bwana unisikilize, mahangaiko ya dunia mengi sana, yamenisonga kushoto hata kulia, mbele mbele na nyuma mimi sioni kitu
Ndugu zangu nao wananichekelea, ninapopambana na hali hali zangu, hivyo tumaini langu naliweka kwako, njoo hima Bwana wangu uniokoe
top of page
bottom of page
Comentarios