Nipishe njia nipeni nafasi- Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi nitamwimbia ngoma nitacheza- Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi Natamani kuruka, nifika kule, Nimuinue Mungu kwa mikono yangu, Nimueleze kwa kinywa, changu mwenyewe, Kwamba nimefurahi kwa upendo wake, Bwana nashukuru, nashukuru nashukuru tu Ninashukuru kwa kunipenda bila mwisho, Sina cha kusema, cha kusema cha kusema tu, Ninashukuru kwa kunipenda bila mwisho
Kaniinua kutoka shimoni -Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi akaniweka juu ya kinara - Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi
Nitazunguka kwa maringo tele - Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi na tabasamu lisilo kauka - Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi
Nitawashika wenzangu mikono - Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi tujiinue juu kwa pamoja -Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi
Wenzangu si mmejionea wenyewe - Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi, Mungu alivyo mwema wa ajabu -Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi
Nitaandika utukufu wake - Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi na wajukuu wangu wausome -Nimuonyeshe Mungu nilivyofurahi
top of page
bottom of page
Comments