Nipe Biblia nyota ya furaha, wapate nuru wasafirio;
Hakuna la kuzuia amani, Kwani Yesu alituokoa.
Nipe Biblia neno takatifu, Nuru yako itaniongoza,
Sheria na ahadi na upendo, Hata mwisho vitaendelea.
Nipe Biblia nihuzunikapo ikinijaza moyoni dhambi ;
Nipe neno zuri la Bwana Yesu, Nimwone Yesu Mwokozi wangu.
Nipe Biblia nipate kuona, hatari zilizo duniani;
Nuru ya neno lake Bwana Yesu, Itaangaza njia ya kweli.
Nipe Biblia taaa ya maisha; Mfariji tunapofiliwa;
Unionyeshe taa ya mbinguni, Nione utukufu wa Bwana
Comments