top of page

Nipe Biblia

Nipe Biblia nyota ya furaha, wapate nuru wasafirio;

Hakuna la kuzuia amani, Kwani Yesu alituokoa.


Nipe Biblia neno takatifu, Nuru yako itaniongoza,

Sheria na ahadi na upendo, Hata mwisho vitaendelea.


Nipe Biblia nihuzunikapo ikinijaza moyoni dhambi ;

Nipe neno zuri la Bwana Yesu, Nimwone Yesu Mwokozi wangu.


Nipe Biblia nipate kuona, hatari zilizo duniani;

Nuru ya neno lake Bwana Yesu, Itaangaza njia ya kweli.


Nipe Biblia taaa ya maisha; Mfariji tunapofiliwa;

Unionyeshe taa ya mbinguni, Nione utukufu wa Bwana

1 view0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page