Nahangaika hapa duniani, maisha yangu hayana furaha Najua wazi hapa si nyumbani, bali njia ya kupita Niongoze vyema Maria, maria Mwema, Bondeni huku niliko nifike kwa usalama Mbinguni kwa Yesu mwanao
Vita na shari vyote vyanisonga, mashaka mengi yaniingia Mwili a roho havina kinga hatari imezidia
Mama Maria ndiwe jibu langu hapa safarini unisaidie Unipombee kwa mwanao Yesu anikinge anilinde
Kwa kuwa Yesu ni Mwokozi wangu nakusihi Mama Nakusihi sana uzifikishe kwake shida zangu anionee huruma
Kumbuka Mama, Yesu alisema, Mama yangu Mwema Tazama mwanao, nawe Yohana huyu ndiye mama yako
top of page
bottom of page
Comentários