top of page

Ninaye Rafiki

Ninaye rafiki naye Alinipenda mbele;

Kwa kamba za pendo lake Nimefungwa milele.

Aukaza moyo wangu, Uache ugeuzi,

Ninakaa ndani yake, Yeye Kwangu, milele.


Ninaye Rafiki ndiye, Aliyenifilia;

Alimwaga damu yake, Kwa watu wote pia.

Sina kitu mimi tena, Nikiwa navyo tele,

Pia vyote ni amana, Ndimi wake milele.


Ninaye Rafiki naye, Uwezo amepewa;

Atanilinda mwenyewe, Juu `tachukuliwa;

Nikitazama mbinguni, Hupata nguvu tele;

Sasa natumika chini, Kisha juu milele.


Ninaye Rafiki naye, Yuna na moyo mwema;

Ni Mwalimu, Kiongozi, Mlinzi wa daima;

Ni nani wa kunitenga, Na mpenzi wa mbele?

Kwake nimetia nanga, ndimi wake milele.

5 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page