Ninakuabudu Mungu wangu Unayejificha altareni Ninakutolea moyo wangu Usiofahamu siri yako
Mafahamu yangu yadanganya Yanapokuona na kugusa Namsadiki Yesu hadanganyi Yeye Mungu Mwana na Ukweli
Waficha umungu msalabani Na ubinadamu altareni Nami naungama yote mbili Kama mwivi yule mwenye toba
Tomaso aligusa majeraha Nami nasadiki bila shaka Ewe Yesu nipe pendo lako Tumaini kwako na imani
Umeteswa nini Bwana mwema Kwaku nipa mkate wauzima Yesu unifiche ndani yako Ili nilionje pendo lako
Yesu pelikane nitazame Na kwa damu yako nitakase Tone moja ndilo linatosha Na dunia yote yaokoka
Ndani ya mafumbo Yesu yumo Atafumbuliwa kwangu lini NikuoneYesu usowako Nishiriki nawe heri yako AMINA.
top of page
bottom of page
Comments