Nimekombolewa na Yesu na sasa nimefurahi;
Kwa bei ya mauti yake mimi ni mtoto wake.
Kombolewa! Nakombolewa na damu;
Kombolewa! mimi mwana wake kweli.
Kukombolewa nafurahi, kupita lugha kutamka;
Kulionyesha pendo lake, mimi ni mtoto wake.
Nitamwona Mfalme wangu, katika uzuri wake;
Ambaye najifurahisha katika torati yake.
Najua taji imewekwa mbinguni tayari kwangu;
Muda kitambo atakuja, ili alipo, niwepo.
Comments