top of page

Nilipotoka kabisa

Nilipotoka kabisa, sasa narudi;

Nikakawia dhambini, Bwana narudi.


Narudi nyumbani: daima kwako.

Kwa upendo nipokee: Naja nyumbani.


Nikasusurika sana, sasa narudi;

Mwenye uchungu natubu, Bwana narudi.


Nimechoka maovuni, sasa narudi;

Pendo lako lanivuta, Bwana narudi.


Ndilo tumaini langu, sasa narudi;

Yesu alinifilia, Bwana narudi.


Damu yake yanitosha, sasa narudi;

Unioshe kenyekenye, Bwana narudi.

28 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page