(Nikupe nini wewe, Bwana Mungu wangu) x2.
(Kwa mema mengi ee Bwana, unayonitendea mimi maishani Mwangu) x2
Umenilinda wiki nzima - Baba nashukuru, Afya ya mwili na ya roho - Baba umenipa
Umenijalia watoto - Baba nashukuru, Kazi na mali umenipa - Baba nashukuru
Pumzi ya bure umenipa - Baba nashukuru, Kwa vita njaa na magonjwa - Umeniwezesha.
Nikiwa safarini Bwana - Unaniongoza, Waniepusha na ajali - Baba nashukuru.
Akili pia na imani - Umenizidishia, Sauti nzuri umenipa - Nikuimbie wewe.
留言