Nikupe nini ee Mungu cha kukupendeza Uwezo wangu mdogo Bwana waujua pamoja na dhiki inayonisonga Pokea zawadi yangu hii duni
Nikitazama wenzangu wanakutolea Zawadi nyingi na nzuri za kukupendeza kasoro mimi tu natoa kidogo Wakati mwingine sitoi kabisa
Maisha yangu ya dhiki Bwana wayajua Unyonge na udhaifu wangu waujua Sina kitu mimi cha kukutolea Lakini pokea nafsi yangu Bwana
Nayakabidhi maisha yangu kwako Bwana Uniongoze katika njia za uzima unisaidie wakati wa shida Kwani ni wewe tu tumaini langu
Kutoa ndugu ni moyo sio utajiri Ukimtolea Mungu atakuongeza uwasaidie watu maskini Wasiojiweza utabarikiwa
Ninawasihi wenzangu mliojaliwa Maisha bora mazuri na ya kuridhisha msimsahau Bwana Mungu wenu Toeni kwa wingi mtabarikiwa.
コメント