Nikulipe nini ewe Mungu Baba wa Mbinguni Kwani mtu mimi sina kitu cha kujivunia
Nikufananishe na nini humu ulimwenguni Uliumba vyote bahari mito hata milima
Ningekuwa ndege hakika ningeruka angani Ningekuwa nyota ningemulika dunia yote
Nitakutendea nini ili nikufurahishe, Nitakuimbia wimbo gani Baba nikusifu
Unitume Baba popote nipeleke ujumbe Nitalihubiri Jina lako daima milele
top of page
bottom of page
Comments