Nikiziangalia mbingu, ni kazi ya vidole vyako, mwezi na nyota za mbinguni ulizo ratibisha wewe x2
Naye mtu ni kitu gani, hata naye umkumbuke, naye binadamu ni nani, hata naye umuangalie.
Umemfanya punji ndogo, ni mdogo kuliko Mungu, umemvika taji yake, taji ya utukufu na heshima.
Umemtawaza juu ya kazi, ni kazi ya mikono yako, umevitia vitu vyote, chini ya miguu yako ee Bwana.
Kondoo nao ngombe wote, pia wanyama wa kondeni ndege wote wa angani na samaki wote, wote baharini.
Comentários