top of page

Niambie, Ee Mlinzi

Niambie, Ee mlinzi, Umepambazuka je!

Utukufu wa Zayini, Pana dalili zake?

Msafiri uondoke, Utazame mbinguni,

Kiunoni ujifunge, Ni kucha alfajiri.


Mlinzi inamulika Nuru njiani mwako,

Dalili za kuja kwake, Kwamba siku karibu;

Panda itakapolia Itawaamsha wafu,

Watakatifu wa Mungu, Kuwapa kutokufa.


Mlinzi, ione nuru Ya mwaka wa Sabato;

Sauti zinatangaza Ufalme ni karibu;

Msafiri ninaona Mlima wa Zayuni,

Mji wa Yerusalemi Nayo fahari yake.


Kwenye mji wa dhahabu Anaketi mfalme

Katika kiti kizuri: huku anatawala.

Pana amani po pote, Mashamba husitawi;

Na ardhi ina rutuba; Mito ni mitulivu.


Mlinzi, twaribia Nchi iliyo nzuri;

Twende mbele, tufurahi, Nchi inachangamka,

Sikieni kuna wimbo Wa waliookoka;

Kaza mwendo, Ujiunge Na kundi Kubwa hili.

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page