Ni Maria Mtakatifu - Tumshangilie Maria
Ni mzazi wa Mungu mwana - Tumshangilie Maria
Ni mkuu wa mabikira - Tumshangilie Maria
Ni Mama yake Yesu Kristu- Tumshangilie Maria
Vigelegele vifijo na makofi……Hoi hoi nderemo (nyingi) pia vifijo tumshangilie, Mama Maria. Yeye ni mwombezi (wetu) na msaada budi tumwimbie, chereko mama
Mama wa neema ya Mungu- Tumshangilie Maria
Mama Mtakatifu sana- Tumshangilie Maria
Mama wa usafi wa moyo - Tumshangilie Maria
Ni Mama asiye na doa - Tumshangilie Maria
Ni Mama asiye na dhambi - Tumshangilie Maria
Ndiye Mama mpendelevu - Tumshangilie Maria
Ni Mama mstaajabivu- Tumshangilie Maria
Ni Mama wa shauri jema - Tumshangilie Maria
Ndiye Mama wake muumba - Tumshangilie Maria
Ndiye Mama wa Mkombozi- Tumshangilie Maria
Bikira wa utaratibu- Tumshangilie Maria
Ni Bikira mwenye heshima - Tumshangilie Maria
Ndiye Bikira mwenye sifa- Tumshangilie Maria
Ndiye Bikira mwenye enzi - Tumshangilie Maria
Ni Bikira mwenye huruma - Tumshangilie Maria
Na ndiye Bikira amini - Tumshangilie Maria
Na ndiye kioo cha haki - Tumshangilie Maria
Ni kikao chenye hekima- Tumshangilie Maria
Sababu ya furaha yetu- Tumshangilie Maria
Ndiye chombo chenye neema - Tumshangilie Maria
Ndiye chombo chenye heshima - Tumshangilie Maria
Ni chombo bora cha ibada- Tumshangilie Maria
Ndiye waridi lenye fumbo - Tumshangilie Maria
Ndiye mnara wa Daudi- Tumshangilie Maria
Comments