Ni heri wanaostahili kujongea meza yake Bwana (kupokea x2) mwili wake (mwili wake) na kunywa damu yake x2.
1. Ni heri waliojiweka tayari kupokea mwili wake mtakatifu.
2. Wana heri wote wanaostahili, kujongea kwenye meza yake Bwana.
3. Mwili wake ndiye chakula kamili, hushibisha wale wenye kuupokea.
4. Damu yake ndiyo kinywaji halisi, husafisha wale wenye kuupokea.
5. Nimeitika wito wako ee Bwana, najongea kwako Bwana unipokee.
Comments