1a. Nasikia kelele na vigelegele nauliza kweli kuna nini (leo)
b. Nawaona walio na mavazi mazuri wanavyotembea kwa maringo (leo)
Ni harusi pigeni kelele, ni harusi pigeni makofi, ni harusi tuimbe kwa shangwe na vigelegele tupige
2a. Tazameni bwana anavyopendeza, anavyokanyanga polepole- (sana)
b. Naye bibi harusi anametameta, amepambwa maua- (sana)
3a. Nyanyueni bendera mikononi mwenu, mzipeperushe kwa pamoja- (wote)
b. Simameni tucheze kwa furaha wanapoingia, tuimbe kwa shangwe – (wote)
4a. Ewe bwana harusi mpende mke wako, siku zote umlinde – (vyema)
b. Nawe bibi harusi mheshimu mume wako , siku zote umtunze- (vyema)
Comments