1a: Nguzo yetu hapa kwetu kenya filosofia yetu, amani, upendo, umoja wetu ndiyo nguzo yetu, b: Wananchi , viongozi Kenya tuko na lengo moja, Amani, upendo, umoja wetu tuijenge Kenya.
Pamoja tunaishi, pamoja tunajenga pamoja twaimarika kwa pamoja twajenga Kenya na haki ndio ngao na tena ni mlinzi undugu na ustawi, kwa pamoja twasonga mbele x2
2a: Maadui wanataka sana Kenya tugawanyike kumbuka ya kwamba umoja wetu ndiyo nguzo yetu,
b: Tumeishi hapa kwetu Kenya kama jamii moja, amani, upendo, umoja wetu ndiyo nguzo yetu
3a: Wazalendo kwa pamoja sote, tushikane mikono, elimu, viwanda, kilimo Kenya vikaimarike, b: Wanajeshi kwa pamoja sote, tushikane mikono pamoja tulinde mipaya yetu na wananchi wote.
コメント