Mimi si mkamilifu ni mwanadamu, nawe si mkamilifu ni mwanadamu. Mbona tunakoseana twaumizana lakini tusikubali kuchukiana (njoo)
Amani ni jambo jema na muhimu, (jambo muhimu), inaimarishwa kwa mazungumzo (mazungumzo) ikitetereka ihangaikiwe. Na Imani ni tunda la haki, tuzungumze tutendeane haki, karibu njoo (njoo)
Niwe na moyo mwepesi kuomba radhi, niwe mwenye kuelewa na kusamehe, niwe msahaulifu nikikosewa, na mwenye kukumbuka ninapokosea (njoo)
Mbinguni watafurahi wakiona, tuliokwaruzana tunaongea, na tunamaliza tofauti zetu. (njoo)
top of page
bottom of page
Comments