Tazama mimi ninavyopumua, Tazama mimi nilivyo na nguvu Tazama mimi ninavyopumua, Tazama mimi nilivyo na nguvu Hizo zote - ni neema bure toka kwa Mungu Na mimi leo - ngoja nicheze muone, Nitamsifu ngoja nicheze muone, bila kuchoka - ngoja nicheze muone aee
Tazama mimi nakula na kushiba, Tazama mimi nalala nasinzia Tazama naamka mimi mwenyewe, Tazama tazama ah tazama aa aha
Tazama mimi naweza kuongea, Tazama mimi naimba bila shida Tazama naweza kucheza mwenyewe, Tazama tazama ah tazama aa aha
Nikiugua ona napewa pole, ninapofiwa ndugu mwanifariji Tazama niwapo na shida wanajaa tazama tazama ah tazama aa aha
Nikikosea huwa nasamehewa, nikiudhiwa ndugu mwanitetea Tazama dhuluma haitaniua tazama tazama ah tazama aa aha
Nikifurahi ndugu washerehekea, nikiudhiwa ndugu wasononeka Tazama ninaishi kati ya watu tazama tazama ah tazama aa aha
Na yote haya najaliwa na Mungu, Amenipenda upeo wa upendo Tazama na mimi nitamtukuza, Tazama tazama ah tazama aa aha
Comments