Moyoni mwangu moyoni mwangu nisiposema neno asante nisipokiri wema wa Mungu, ulimi wangu ugandamane na kaakaa na kinywa changu mimi x2
Ninakushuru Baba Mungu wangu kwa mema unayo nitendea Baba, siku zote ninawaza jinsi gani nitalipa nini mimi kwa shukrani
Yote uliyoyatenda juu yangu nashindwa kusimulia Baba yangu, machozi yenye upendo na furaha yamelipamba shavu langu
Leo ninaimba nyimbo za furaha ninageuka kushoto na kulia, nimeamsha vinanda na vinubi asubuhi na mapema ninaimba
Umenishibisha mema ya mbinguni, pendo lako limetua ndani yangu, Furaha imetawala moyo wangu jinsi ninavyokusifu Mungu wangu
Kommentarer