top of page

Nena Mungu

Nena rohoni Yesu, Nena kwa upole

Sema kwangu kwa pendo, ‘Huachwi upweke.‘

Fungua moyo wangu, Nisikie mara;

Jaza roho na sifa, Sifa zako Bwana.


Kila siku unene, Vile kwa upole,

Nong`oneza kwa pole wa pendo:

‘Daima utashinda, Uhuru ni wako.‘

Nisikie maneno; ‘Huachwi upweke.‘


Nena kwa wana wako, waonyeshe njia,

Wajaze kwa furaha, Fundisha kuomba;

Wajifunze kutoa Maisha kamili,

Wahimize ufalme, Tumwone mwokozi.


Nena kama zamani, Ulipoitoa

Sheria takatifu: Niiweke pia;

Nipate kutukuza Wewe Mungu wangu,

Mapenzi yoko tena, Daima kusifu.

1 view0 comments

Comentários

Avaliado com 0 de 5 estrelas.
Ainda sem avaliações

Adicione uma avaliação
bottom of page