Zimetiririka zimetiririka, Zimetiririka neema za Mungu
Zimetiririka, neema zimetiririka, neema zimetiririka wote tumeinuliwa aleluya x2
{Majumbani mwetu (zimetiririka) Mashambani mwetu (zimetiririka tiririka) Familia zetu (zimetiririka) tumeinuliwa aleluya} x2
Tazama mimea inavyochanua, hizi ni neema kutoka Mbinguni
Tazama bahari na mawimbi yake, vinashangilia neema za Mungu
Tazama wanyama wanavyopendeza, ndege wa angani wanaburudisha
Mvua inanyesha jua inawaka, kuukamilisha utukufu wake
Mchana na usiku vinatuongoza, kuyafurahia majira ya mwaka
Mbingu zafurahi na mawingu yote, vinashangilia neema za Mungu
Comments