Leteni ndama walionona madhabahuni kwa Bwana (tena) toeni bila ya kinyongo moyoni ndipo mtabarikiwa naye x2
Leteni ndama walioshiba majani ya kondeni, mkamtolee Mungu Baba yetu wa mbinguni.
Peleka vipaji vyako vilivyo safi na vyakupendeza, ndipo utakapokitikisa kiti cha Mwenyezi
Kumbuka yule mjane , alitetoa senti moja, alibarikiwa na kuongezewa na Mungu Baba.
Sadaka iliyo safi ni ile inayokugusa wewe, hivyo ndivyo sadaka iliyo safi kwa Mungu.
Isaka alitolewa na baba yake kama sadaka, hivyo Abrahamu alizidishiwa uzao wake.
Comments