BASS: Nawapa amri
ALL: Amri pendaneni, (asema Bwana) (kama vile mimi nilivyowapenda ninyi, (nanyi), nanyi pia pendaneni) x2
Wapenzi na tupendane, neno latoka kwa Mungu, na pia apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu, tupendane.
Yule asiye na pendo hakumjua Mungu wetu, kwa maana Mungu ni mwenye upendo kamili, naye ametuamuru, tupendane.
Mungu apenda dunia, kwa mapendo yake kwetu, akamtuma Mwanaye, Mwana wake wa pekee, hapa kwetu duniani, tupendane.
Comments