Nataka Imani hii: Imani imara,
Ambayo haitetemi Kitu chote
Wakati wa shida,
Wakati wa shida.
Isiyonung`unika Huzuni, taabu;
Lakini katika saa ya matata
Humwamini Mungu,
Humwamini Mungu.
Imani inayo ng`aa katika tufani;
Isiyoogopa giza, wala shida,
Njaa na Hatari,
Njaa na hatari.
Haiogopi dunia, Kudharau kwake;
Haiangushwi na hila, na uwongo
Dhambi na ogofyo,
Dhambi na ogofyo.
Bwana, nipe imani hii, Hivi nitaweza
Kuonja hapa chini ulimwenguni,
Kurithi furaha,
Kurithi furaha.
Comments