Nasikia kelele na vigelegele nauliza
kwani kuna nini (leo). Nawaona walio
na mavazi mazuri wanavyotembea kwa
mariongo tele (leo).
Ni harusi pigeni kelele. Ni harusi pigeni
makofi. Ni harusi tuimbe kwa shangwe,
na vigelegele tupige x2.
Tazameni bwana anavyopendeza,
anavyokanyanga polepole (sana).
Naye bibi harusi anametameta,
anapambwa mavazi mazuri (sana).
Nyanyueni bendera mikononi mwenu
muzipeperushe kwa pamoja (wote).
Simameni tucheze kwa furaha,
wanapoingia, tuimbe kwa shangwe (wote).
Tuwafurahieni ndugu zetu hawa
walioamua kufunga (ndoa).
Ndoa ni maagizo yake Mungu Baba
kwa upendo wasivunje hiyo (ndoa).
Ewe bwana harusi umpende mke wako
siku zote umlinde (vyema).
Naye bibi harusi mheshimu mume wako
siku zote umtunze (vyema).
Comentarios