Nani ni nani, ni nani ni nani, ni nani ni nani, nani kama Mungu Mwenye uwezo, na mwenye ukuu ni nani ni nani nani kama Mungu
1. Ameniumba, jinsi nilivyo, nipendezavyo ni nani kama Mungu Niseme nini, niimbe nini, nilie vipi, ni nani kama Mungu
2. Tazama jua, mwezi na nyota, mbingu na nchi . . . Nao usiku, jua li wapi, ni maajabu ni nani kama Mungu
3. Ananilinda, mchana kutwa, pia usiku, ni nani kama Mungu Nikitembea, nikisimama, ananilinda , ni nani kama Mungu
4. Tazama ndege wa msituni wanavyoishi , ni nani kama Mungu Hawana shamba wala vilenge anawalisha , ni nani kama Mungu
5. Na maarifa, tuliyonayo, yeye katupa, ni nani kama Mungu Njooni pamoja, tumuimbie, na tumsifu, ni nani kama Mungu
Comentarios