Nakukaribisha Yesu wangu, ukae moyoni mwangu (Bwana) nakukaribisha Yesu wangu chakula chenye uzima x2
Nishibishe kwa chakula cha uzima, uninyweshe kinywaji safi cha roho
1. Mwili wako ni chakula kinachoiburudisha roho yangu,
Yesu karibu moyoni mwangu, ukae nami daima.
2. Damu yako ni kinywaji kinachoiburudisha roho yangu,
Yesu karibu moyoni mwangu, ukae nami daima.
3. Kwa mwili na damu yako Ee Yesu tunapata uzima tele
Yesu karibu moyoni mwangu ukae nami daima
Comments