Nakuja mbele zako Bwana, ninakuja na zawadi yangu,
ingawa ni kidogo (sana) Bwana uipokee x2
Nimekaa mimi nimejiuliza moyoni nitaenda je mbele za Bwana kwani Bwana amenilinda mimi salama amezibariki kazi zangu
Mungu Baba, pokea nilichonacho
Ninatoa kwa moyo mkunjufu pokea hiki kidogo nilichonacho.
Haya yote ni kwa ajili yako pokea uzidi kunijalia mema Ninaleta, mbele ya altare yako
Mkate na Divai twaleta pokea, vigeuze mwili pia damu Hata fedha zetu za mifukoni twakupa, zote ni mali yako e Bwana Tubariki, tupokee mbele zako.
Comments