Naja kwako nipokee ingawa mimi ni mdhambi x2
Sadaka naleta japo mi sifai,
Ewe Mungu Baba ipokee,
Mkate divai zao la mashamba,
Mbele yako Bwana twaleta.
Kazi zetu zote fedha zetu zote,
Mbele zako Bwana twaleta,
Nia zetu zote shida na furaha
Mbele yako Bwana twaleta.
Familia zetu kanisa na nchi,
Twazileta kwako ee Baba,
Twakuomba Baba utupe amani,
Imani pia na mapendo
Shukurani zetu tunakutolea,
Twakuomba Baba pokea,
Nazo nyoyo zetu nazo nia zetu,
Kwako Mungu Baba twaleta
Naja mbele yako ewe Mungu wangu,
huku nimejawa na dhambi.
Unihurumie uniwie radhi
mbele yako Baba natubu.
Comments