Mimi ndimi mzabibu wa kweli, Mimi ni mzabibu wa kweli nanyi m matawi yangu, asema Bwana x2
Na Baba yangu ndiye mkulima, kila tawi lisilozaa, Baba hulikata nalo tawi lizaalo, Baba hulisafisha, ili lizidi kuzaa
Kaeni nyote ndani yangu mimi, nami nikae ndani yenu, kwa maana mtu akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo huzaa matunda
Mimi ni mti mti wa zabibu, nanyi ndinyi matawi ya mzabibu huu, tawi linalojitenga, kutoka kwa mti huu, hunyauka tena hufa
Comments