Mwumbaji, Mfalme, Vitu vyote vyako;
Ni kwa ukarimu wako; Ninabarikiwa,
Ni kwa ukarimu wako, Ninabarikiwa.
Uliyeniumba, Nakutegemea;
Sina budi kuzisifu Hisani zako kuu,
Sina budi kuzisifu Hisani zako kuu.
Nitatoa nini? Kwanza vyote vyako,
Upendo wako wadai Moyo wa shukrani,
Upendo wako wadai Moyo wa shukrani.
Nipewe neema, Niwe na uwezo
Wa kuishi kwako, Bwana: Siku zangu,zako,
Wa kuishi kwako, Bwana: Siku zangu,zako.
Comments