Nimemuona yule ninayemtafuta na neema zake, nimemuona leo nimemuona Mungu) x2. Mkononi mwake ana uzima tena ni wa milele, mkononi mwake ana uzima ninaoutafuta, na uzima huo anatoa bure kwa walio tayari, lakini kuna kanuni moja ya kwamba, uwajali watu.
Nimemuona Mungu yu mtupu u hana nguo - anatamani mimi niende nikamvishe
Nimemuona Mungu ana njaa hana chakula- anatamani mimi niende nikamlishe
Nimemuona Mungu ni mgonjwa a kitandani- anatamani mimi niende kumtazama
Nimemuona Mungu amefungwa a gerezani- anatamani mimi niende kumfariji
Nimemuona Mungu ni mkimbizi mpakani- anatamani mimi niende kumpokea
Nimemuona Mungu ni yatima hana wazazi- anatamani mimi niende nikamtunze
Nimemuona Mungu ni mjane hana matunzo- anatamani mimi niende kumhifadhi
Nimemuona Mungu amefiwa ana majonzi- anatamani mimi niende kumfariji
Nimemuona Mungu ni kilema na hajiwezi- anatamani mimi niende kumuinua
Nimemuona Mungu atolewa angali mimba- anatamani mimi niende kumtetea
Nimemuona Mungu anapigwa kwa makombora- anatamani mimi niende suluhisha
Nimemuona Mungu ni mtumwa ananyanyaswa- anatamani mimi niende kumtetea
top of page
bottom of page
Comments