Mungu atukuzwe kwa mambo makuu,
Upendo wake ulitupa Yesu,
Aliyejitoa maisha yake,
Tuwe nao uzima wamilele.
Msifu, msifu, dunia sikia;
Msifu, msifu, watu wafurahi;
Na uje kwa Baba, kwa yesu Mwana,
Ukamtutukuze kwa mambo yote.
Wokovu kamili, zawadi kwetu,
Ahadi ya Mungu kwa ulimwengu;
Wanaomwamini na kuungama,
Mara moja wale husamehewa
Alitufundisha mambo makuu,
Alihakikisha wokovu wetu,
Lakini zaidi, ajabu kubwa,
Yesu atakuja na tutamwona.
Comments