top of page

Mungu Nawe Nanyi

Mungu nawe nanyi daima; hata twonane ya pili,

Awachunge kwa fadhili, Mungu nawe nanyi daima.


Hata twonane juu, hata twonane tena kwake;

Hata twonane juu, Mungu nawe nanyi daima.


Mungu nawe nanyi daima; awafunike mabawa,

Awalishe, awakuze; Mungu nawe nanyi daima.


Mungu nawe nanyi daima; kila wakati wa shida

Awalinde hifadhini; Mungu nawe nanyi daima.


Mungu nawe nanyi daima; awabariki na pendo

Ambalo halina mwisho; Mungu nawe nanyi daima.

0 views0 comments

コメント

5つ星のうち0と評価されています。
まだ評価がありません

評価を追加
bottom of page