Mungu Msaada wetu tangu miaka yote;
Ndiwe tumaini letu la zamani zote.
Kivuli cha kiti chako ndiyo ngome yetu,
Watosha mkono wako ni ulinzi wetu.
Kwanza havijakuwako nchi na milima,
Ndiwe Mungu; chini yako twakaa salama.
Na miaka elfu ni kama siku moja kwako;
Utatulinda daima, tu wenyeji wako.
Bwana msaada wetu tangu miaka yote,
Mlinzi wetu na ngome, daima, milele.
Comments