Msingi wa Kanisa Ndiye Yesu Bwana;
Kiumbe chake kipya Akipenda sana;
Kutaka ‘kitafuta Alishuka chini,
Naye kwa haja yake, Akafa Mtini.
Lina kila kabila Kisha ndiyo moja
Wokovu wake una Mwokozi ndiyo moja;
Uzazi ni umoja. Moja tumaini.
Chakula ni kimoja. Moja tumaini.
Watu hustaajabu Kwa mashaka yote.
Yaipatayo nje Hata ndani mwote;
Ila watakatifu Humwomba, wakikesha
Usiku ni kilio. Asubuhi raha.
Mashaka na taabu Hata vita vyake.
Vyangoja matimizo Ya amani yake.
Ndipo kwa macho yetu Twone utukufu
Kanisa ya kushinda itastarehe juu.
Comments