top of page

Msingi wa Kanisa

Msingi wa Kanisa Ndiye Yesu Bwana;

Kiumbe chake kipya Akipenda sana;

Kutaka ‘kitafuta Alishuka chini,

Naye kwa haja yake, Akafa Mtini.


Lina kila kabila Kisha ndiyo moja

Wokovu wake una Mwokozi ndiyo moja;

Uzazi ni umoja. Moja tumaini.

Chakula ni kimoja. Moja tumaini.


Watu hustaajabu Kwa mashaka yote.

Yaipatayo nje Hata ndani mwote;

Ila watakatifu Humwomba, wakikesha

Usiku ni kilio. Asubuhi raha.


Mashaka na taabu Hata vita vyake.

Vyangoja matimizo Ya amani yake.

Ndipo kwa macho yetu Twone utukufu

Kanisa ya kushinda itastarehe juu.

8 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page