Mshukuruni Mwokozi enyi mataifa, pigeni vigelegele pigeni makofi x 2
Tangazeni rehema zake hekaluni mwake, semeni ya kuwa Bwana ni mwenye adili x 2
Njoni tumwimbie Bwana mwamba wa wokovu wetu, mikononi mwake zimo bonde za dunia
Bahari ni yake ndiye aliyeumba na mikono yake ilituumba sisi
Bwana ametamalaki mataifa yatetema, ameketi juu ya makerubi mbinguni
Yeye Bwana katika sayuni ni mkuu, katukuka juu ya mataifa yote.
Mshangilieni Bwana, mwimbieni na zaburi, vinanda na baragumu vyote mvipige
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, kwa kuwa fadhili zake ni za milele
Comments